Lengo na Madhumuni

Lengo
Lengo kuu la MKURABITA ni kuwawezesha wanaomiliki rasilimali na biashara katika sekta isiyokidhi matakwa ya sheria (mfumo usio rasmi) kuingia katika sekta rasmi ili kushiriki kikamilifu katika mfumo wa kisasa wa uchumi wa soko; na itakayowawezesha kuboresha biashara na kupunguza umaskini wa kipato katika kaya na kukuza uchumi kitaifa.

Madhumuni
Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa mfumo wa kitaifa wa umiliki rasilimal (Ardhi na majengo) na uendeshaji biashara utakaoboresha kanuni na taratibu za kijamii na kuzioanisha na sheria zilizorekebishwa ili kuwa na mfumo mmoja wa kisheria na kitaasisi ambao utatumiwa na walengwa kurasimisha rasilimali na biashara zao; kisha kuzitumia kupata mitaji ya kugharamia shughuli zao kadri ya utashi wao. Kwa kuwa washiriki katika uchumi wa soko la ndani na nje ya nchi.

Madhumuni ya MKURABITA ni pamoja na;

  • Kuandaa na kusimamia mfumo mmoja wa kitaifa wa umiliki rasilimali, Ardhi na majengo na uendeshaji biashara utakaotumika na makundi mbalimbali ya jamii nchini. Mfumo huu utawezesha kuratibu na kupunguza ukubwa wa sekta isiyo rasmi katika umiliki na utumiaji rasilimali, uanzishaji na uendeshaji biashra.
  • Kuimarisha umoja kitaifa kwa kuunganisha sekta isiyo rasmi na sekta rasmi katika uchumi na hivyo kurahisisha juhudi za serikali katika kusimamia uchumi wa taifa.
  • Kuwezesha rasilimali za wanyonge zinazomilikiwa nje ya mfumo rasmi kusajiliwa na kutambuliwa rasmi katika mfumo mpya wa kisheria ili ziweze kutumika kupata mitaji.
  • Kuandaa utaratibu unaowawezesha viongozi wa jadi na jamii pamoja na wanyonge walio katika sekta isiyo rasmi kuyaafiki mabadiliko haya yatakayoingiza umiliki wa rasilimali na biashara zao katika mfumo mmoja wa kitaifa wa umiliki mali na biashara ili wamiliki waweze kunufaika na fursa zilizopo kwenye uchumi wa kisasa wa soko huria.
  • Kuwezesha utekelezaji wa maboresho mbalimbali ya kiuchumi na fedha mara wadau wote watakapoingia katiak mfumo mmoja wa soko
  • Kulinda maslahi ya wanyonge nchini Tanzania yasiathiriwe na migongano ya utandawazi
 

 
 
  • Hakikisha kuwa mipaka ya kijiji imehakikiwa na kupimwa ipasavyo ili kuepusha migogoro ya mipaka na vijiji jirani
  • Kijiji kiwe kimesajiliwa na kupata Cheti cha Ardhi ya Kijiji
  • Kijiji kiwe na jengo linalofaa kwa Masjala ya ardhi ya Kijiji
  • Maombi ya kupimiwa na kupata hati miliki ya kimila yapelekwe kwenye Halmashauri ya Kijiji kwa ajili ya mapendekezo ya kuidhinishwa
  • Maombi lazima yapitishwe na kuidhinishwa na Mkutano Mkuu wa Kijiji
 
 
  • Kutambuliwa na kuainishwa kwa eneo la urasimishaji na Halmashauri husika katika mji, Manispaa au Jiji,
  • Uhamasishaji kwa Uongozi na wananchi wa eneo la urasimishaji,
  • Utayarishaji wa michoro ya mipango miji na kuidhinishwa na mamlaka husika,
  • Upimaji ardhi ya wananchi kulingana na michoro ya mipango miji
  • Uidhinishaji wa ramani za upimaji kwenye mamlaka husika,
  • Utayarishaji na utoaji wa Hati za kumiliki ardhi kwa wamiliki wa ardhi iliyopimwa.
 

   
 
Jumla 17848