Utangulizi

Mpango wa Kurasimisha Rasimali na Biashara za wanyonge Tanzania (MKURABITA) ni mpango ulioanzishwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ukilenga kuwapanguvu kiuchumi, wananchi hasa wale wa kipato cha chini (wanyonge) vijijini na mijini, kwa kuwaongezea uwezo wa kumiliki rasilimali nakufanya biashara katika mfumo rasmi wa kisasa, unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria na kanuni rasmi za kiutawala.

Mpango huu ni sehemu ya Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini Tanzania (MKUKUTA), na zaidi inalenga kuwezeshauhamishaji wa rasimali na biashara za walengwa, kutoka kwenye sekta isiyo rasmi, kwenda kwenye sekta rasmi, kama njia mojawapo ya kupiga vita umaskini na kuendeleza uchumi wa kitaifa wa soko huria. MKURABITA iko katika Ofisi ya Rais.


 
 
  • Hakikisha kuwa mipaka ya kijiji imehakikiwa na kupimwa ipasavyo ili kuepusha migogoro ya mipaka na vijiji jirani
  • Kijiji kiwe kimesajiliwa na kupata Cheti cha Ardhi ya Kijiji
  • Kijiji kiwe na jengo linalofaa kwa Masjala ya ardhi ya Kijiji
  • Maombi ya kupimiwa na kupata hati miliki ya kimila yapelekwe kwenye Halmashauri ya Kijiji kwa ajili ya mapendekezo ya kuidhinishwa
  • Maombi lazima yapitishwe na kuidhinishwa na Mkutano Mkuu wa Kijiji