| |
|
|
|
|
|
|
| |
| |
Mpango wa kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) unatekelezwa kupitia awamu kuu nne ambazo ni pamoja na;
- Tathmini ya sekta isiyo rasmi
- Maandalizi ya Maboresho
- Utekelezaji wa Maboresho
- Kuimarika kwa Mitaji na Utawala Bora
|
|
|
| |
- Hakikisha kuwa mipaka ya kijiji imehakikiwa na kupimwa ipasavyo ili kuepusha migogoro ya mipaka na vijiji jirani
- Kijiji kiwe kimesajiliwa na kupata Cheti cha Ardhi ya Kijiji
- Kijiji kiwe na jengo linalofaa kwa Masjala ya ardhi ya Kijiji
- Maombi ya kupimiwa na kupata hati miliki ya kimila yapelekwe kwenye Halmashauri ya Kijiji kwa ajili ya mapendekezo ya kuidhinishwa
- Maombi lazima yapitishwe na kuidhinishwa na Mkutano Mkuu wa Kijiji
|
|
|
| |
- Kutambuliwa na kuainishwa kwa eneo la urasimishaji na Halmashauri husika katika mji, Manispaa au Jiji,
- Uhamasishaji kwa Uongozi na wananchi wa eneo la urasimishaji,
- Utayarishaji wa michoro ya mipango miji na kuidhinishwa na mamlaka husika,
- Upimaji ardhi ya wananchi kulingana na michoro ya mipango miji
- Uidhinishaji wa ramani za upimaji kwenye mamlaka husika,
- Utayarishaji na utoaji wa Hati za kumiliki ardhi kwa wamiliki wa ardhi iliyopimwa.
|
|
|
|
|