MKURABITA ni nini?

Lengo
Kuwawezesha walengwa ambao ni makundi au watu binafsi wanaomiliki rasilimali na kuendesha biashara zao katika mfumo usio rasmi, ili waweze kuingia katika mfumo rasimi na kushiriki kikamilifu katika mfumo wa kisasa wa uchumi wa soko huria

Madhumuni
Kujenga mfumo mmoja wa kanuni za umiliki wa mali na biashara utakaounganisha na kuboresha kanuni zinazotumiwa na makundi mbambali ya jamii nchini ili kuunda mfumo mmoja wa kitaifa wa umiliki mali na biashara


 
 
  • Hakikisha kuwa mipaka ya kijiji imehakikiwa na kupimwa ipasavyo ili kuepusha migogoro ya mipaka na vijiji jirani
  • Kijiji kiwe kimesajiliwa na kupata Cheti cha Ardhi ya Kijiji
  • Kijiji kiwe na jengo linalofaa kwa Masjala ya ardhi ya Kijiji
  • Maombi ya kupimiwa na kupata hati miliki ya kimila yapelekwe kwenye Halmashauri ya Kijiji kwa ajili ya mapendekezo ya kuidhinishwa
  • Maombi lazima yapitishwe na kuidhinishwa na Mkutano Mkuu wa Kijiji