Dhana na Mantiki yake

Mpango huu unalenga wadau wa sekta isiyo rasmi, ambao wengi wao ni wanyonge kiuchumi. Kuingia kwao katika mfumo rasmi wa umilikaji wa mali na uendeshaji wa biashara kutawawezesha kutumia rasilima zao kupata mitaji ya kugharamia shughuli zao za kiuchumi na hivyo kupunguza umaskini ndani ya familia na kuinua uchumi wa nchi.


 
 
  • Hakikisha kuwa mipaka ya kijiji imehakikiwa na kupimwa ipasavyo ili kuepusha migogoro ya mipaka na vijiji jirani
  • Kijiji kiwe kimesajiliwa na kupata Cheti cha Ardhi ya Kijiji
  • Kijiji kiwe na jengo linalofaa kwa Masjala ya ardhi ya Kijiji
  • Maombi ya kupimiwa na kupata hati miliki ya kimila yapelekwe kwenye Halmashauri ya Kijiji kwa ajili ya mapendekezo ya kuidhinishwa
  • Maombi lazima yapitishwe na kuidhinishwa na Mkutano Mkuu wa Kijiji